Amos 2:1-3

1 aHili ndilo asemalo Bwana:

“Kwa dhambi tatu za Moabu,
hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu.
Kwa sababu alichoma mifupa ya mfalme wa Edomu,
ikawa kama chokaa.
2 bNitatuma moto juu ya Moabu
ambao utateketeza ngome za Keriothi.
Moabu ataanguka kwa ghasia kubwa
katikati ya vilio vya vita na mlio wa tarumbeta.
3 cNitamwangamiza mtawala wake
na kuwaua maafisa wake wote pamoja naye,”
asema Bwana.
Copyright information for SwhNEN